Utamaduni wa Mufuliiru

Hali ya kuishi: Mufuliiru anapenda kuishi pamoja na jamaa lake, wote kwa mahali pamoja. Pamoja na hiyo, anajenga pamoja na wengine. Hana ubaguzi kwa watu wengine. Hivyo, anaonekana kuwa jirani mwenye amani.

1. Kazi zake  

a) Ulimaji: Mufuliru anaishi kwa kazi ya ulumaji wa migomba, mihogo, na viazi na aina ingine ya mahole, na mihindi, na karanga, na manjegele, na nyanya, matunguu...

 

 

 

b) Ufugaji

Mufuliru ni mfugaji tangu zamani. Anafuga mifugo ya aina mbali-mbali, kama vile mbuzi, kuku, kondoo, ngombe... Hiyo mifugo yote aliijengea nyumba. Kwa sasa ngombe wanaishi karibu na makao. Ni katika ufugaji ndipo anapata mali. Ngombe   inasaidia kwa kupata mke, mbuzi ni kwa kumaliza mapashwa mengine, na kuku ni kwa kuzimana wakwe na wageni.
  

c) Kufua chumakufanya vyombo vya udongo, na vya mti: Wafuliru walifanya viwanda vya kazi vya hali ya juu. Walifua vyuma na kufanya vyombo vya aina mbali-mbali, kama vile jembe, mikuki, shuma cha kuchimba, mhoro na kazalika. Kazi hiyo ilifanyika ndani ya kiwanda cha kufua. Mufuliiru alifanya vyombo vingi kupitia miti na kuvitumia, kama vile "ndasho", "ndango", karabo", "mitungi", "mubangala", "kibya",  "nakororo".

  

Ndeha.jpg

d) Uwindaji na uvuvi: Mufuliru ni muwindaji sana. Anatumia mkuki na imbwa. Anafanya pia mitego ya aina mbali-mbali. 

Pia Mufuliru ni mvuvi. Katika uvuvi, mara anakausha maji na kwa kukamata sama wala anatumia vifaa vyake vya uvuvi kama vile "migono", tusaaso", "muhunda" na nyavu...pia kutia dawa ya kuua samaki, na kamata na mikono ndani ya maji.


e) Uchuuzi: Mufuliiru anafanya uchuuzi wa mbuzi na ngombe... Anauzisha pia vyombo yenye alifanya kwa mikono yake kama vile jembe, mhoro, visu...


2. Chakula: Chakula chake cha kawaida ni ugali na nyama. Lakini anakula vile-vile vyakula vingine. Mufuliru anakula pia matunda ya aina mbali-mbali, na nyama za mwitu na samaki na uyoga. Lakini hakula kila aina ya nyama ya pori ao ya samaki.


 

3. Kinywaji: Kinywaji chake ni pombe ya ndizi. Anakunywa vile-vile togwa.

 

4. Inyumba: Nyumba yake inajengwa kwa miti na kuezekwa kwa nyasi. Ni nyumba ya mviringo yenyekuwa na chumba moja ndani na sabuleni. 

 

   





5. Utawala: Inchi ya Wafuliiru ni chini ya mutawalammoja. Mwami alisimikwa na kuvalishwa taji ya kifalme. Wafuliiru wanamuheshi sana, wanaheshi na watawala wenye kuwa karibu ya mfalme. Katika Wafuliru hakuna wafalme wawili pia hakuna mwami mke.


6. Vita: Mufuliiru ni shujaa wa vita. Anatumia zaidi fimbo na mkuki. Tangu zamani Mufuliiru alijua kufanya vita kwa kutumia upinde. Hakika, hakuweza kuogopa vita. Lakini ni mtu mpole sana, wala hataki uzushi. Pamoja na hiyo, hataki kugandamizwa.


7. Kuowa: Kijana mwanaume wa Mufuliiru alipewa mke mmoja na baba yake kwa kutowa mali. Lakini alioa zaidi ya mke mmoja. Ndio maana anasema mizali « umushosi aba ku mandu, si ataba ku bundu  », maana yake mwanaume anakula sahani za ugali, wala hakuli sahani ya ugali. Pia anasema « Umundu bali bandu », inamaana mtu lazma awe na watu wengi. Zamani Mufuliiru alipyana mke wa baba yake, alipyana vile-vile mke wa ndugu yake.


8. Matanga: Wakati Mufuliiru anapatwa na maafa, walifanya matanga kwa mda wa siku tano. Na ikiwa alizaa watoto wa mapasha ni siku sita za matanga. Wakati wa kumaliza matanga ilibidi kunyowa nywele kichwani kwa jamaa ile, na kusema maneno ya asili. Katika maneno hiyo ya asili, ikiwa ni baba wa jamaa ndie alikufa walichukua kijana mwanaume ambae ni mkubwa katika jamaa na kumupa mkuki kwa kumusimika kwa nafasi ya baba. Pia walichukua mdogo ya marehemu na kumpa mhoro kwa kuchunga jamaa la marehemu. Ikiwa marehemu aliacha watoto wa kike tu, mkuki hautapatikana hapo inje, wala hawatasimika kiasili. Na kama marehemu alichukuwa mke wa ndugu yake na kuishi naye wakati anapokufa hawatashimika mtoto ambae alizaa kwa mke wa ndugu yake. Kwa wakati huo wa matanga mtu wa jamaa hakuruhusiwa kukoga maji wala kumukaribiya mke wake.


9. Hekima: Hekima ya Mufuliiru inaonekana katika hali yake ya kuzungumuza. Anatumia mizali na maneno ya hekima, na vitendawili. Alijua sana kutoa hadisi.  


10. Nyimbo na kucheza: Mufuliru anajua kuimba na kucheza. Anakuwa na vyombo vyake vya muziki kama vile likimbi, minyanga, ngoma...


Likimbi:   Finyanga hapa ili uone Historiya ya Kifuliru Picha ya Likimbi  
Share