Utamaduni wa Mufuliru
Hali ya kuishi: Mufuliiru anapenda kuishi pamoja na jamaa lake, wote kwa mahali pamoja. Pamoja na hiyo, anajenga pamoja na wengine. Hana ubaguzi kwa watu wengine. Hivyo, anaonekana kuwa jirani mwenye amani.
1. Kazi zake
a) Ulimaji: Mufuliru anaishi kwa kazi ya ulumaji wa migomba, mihogo, na viazi na aina ingine ya mahole, na mihindi, na karanga, na manjegele, na nyanya, matunguu...
b) Ufugaji
Mufuliru ni mfugaji tangu zamani. Anafuga mifugo ya aina mbali-mbali, kama vile mbuzi, kuku, kondoo, ngombe... Hiyo mifugo yote aliijengea nyumba. Kwa sasa ngombe wanaishi karibu na makao. Ni katika ufugaji ndipo anapata mali. Ngombe inasaidia kwa kupata mke, mbuzi ni kwa kumaliza mapashwa mengine, na kuku ni kwa kuzimana wakwe na wageni.
c) Kufua chuma, kufanya vyombo vya udongo, na vya mti: Wafuliru walifanya viwanda vya kazi vya hali ya juu. Walifua vyuma na kufanya vyombo vya aina mbali-mbali, kama vile jembe, mikuki, shuma cha kuchimba, mhoro na kazalika. Kazi hiyo ilifanyika ndani ya kiwanda cha kufua. Mufuliiru alifanya vyombo vingi kupitia miti na kuvitumia, kama vile "ndasho", "ndango", karabo", "mitungi", "mubangala", "kibya", "nakororo".
d) Uwindaji na uvuvi: Mufuliru ni muwindaji sana. Anatumia mkuki na imbwa. Anafanya pia mitego ya aina mbali-mbali.
Pia Mufuliru ni mvuvi. Katika uvuvi, mara anakausha maji na kwa kukamata sama wala anatumia vifaa vyake vya uvuvi kama vile "migono", tusaaso", "muhunda" na nyavu...pia kutia dawa ya kuua samaki, na kamata na mikono ndani ya maji.
e) Uchuuzi: Mufuliiru anafanya uchuuzi wa mbuzi na ngombe... Anauzisha pia vyombo yenye alifanya kwa mikono yake kama vile jembe, mhoro, visu...
2. Chakula: Chakula chake cha kawaida ni ugali na nyama. Lakini anakula vile-vile vyakula vingine. Mufuliru anakula pia matunda ya aina mbali-mbali, na nyama za mwitu na samaki na uyoga. Lakini hakula kila aina ya nyama ya pori ao ya samaki.
3. Kinywaji: Kinywaji chake ni pombe ya ndizi. Anakunywa vile-vile togwa.
4. Inyumba: Nyumba yake inajengwa kwa miti na kuezekwa kwa nyasi. Ni nyumba ya mviringo yenyekuwa na chumba moja ndani na sabuleni.
Copyright © 2022, Vyuka, uyitoneese!